• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

DC CHATO AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: February 25th, 2023


Mkuu wa wilaya ya Chato Mhe


Deusdedith Katwale ameitoa kauli hiyo mapema leo hii katika Kata ya Bwanga ambako zoezi la kufanya usafi wa mazingira kiwilaya limefanyika ikiwa ni Jumamosi ya Mwisho wa Mwezi kama ambavyo tumejiwekea utaratibu huo kama taifa na sasa ni desturi yetu kama watanzania.


Aidha Mhe. Katwale amewataka wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha na kuhakikisha wanafanya usafi katika maeneo yao ameongeza kwa kusema, "haina maana mimi na timu yangu mpaka nitoke Chato kuja kukwambia fanya usafi katika eneo lako wakati wewe mwenyewe unaona hali halisi na kuanzia sasa kila mmoja aone kuwa usafi ni jambo ambalo huwezi kulitenganisha na maisha ya mwanadamu"


Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chato Ndg. Mandia Kihiyo amemshukuru Mhe. Mkuu wa wilaya kwa kuwa tayari kuja kushiriki katika usafi pamoja na watumishi wa umma na wananchi wa Bwanga uliofanyika katika Soko la Bwanga ambapo mwitikio umekuwa mkubwa jambo ambalo linaashiria sasa wana Bwanga na Chato kwa ujumla wameamua kufanya kazi kama timu moja.


Pia ameongeza kwa kusema Chato hatuna magonjwa ya milipuko kama ilivyo katika maeneo mengine jambo ambalo ni matunda ya kuweka maeneo yetu kuwa safi kwani usafi ni afya.


Mhe Diwani ya Kata ya Bwanga amemkaribisha Mhe. Mkuu wa wilaya ya katika Kata hiyo huku akimuahidi yeye pamoja na wana Bwanga wapo tayari kumpa ushirikiano mda na wakati wowote atakapohitaji.


Katika hatua nyingine Mhe Diwani amemwomba Mhe. Mkuu wa wilaya kuangalia namna ya kufanya maboresho ya soko la Bwanga kwani limekuwa finyu na kupendekeza kujengewa Soko la Ghorofa.


Akihitimisha zoezi hilo la usafi Mkuu wa wilaya ya Chato Mhe. Deusdedith Katwale amewataka kila mwananchi kutimiza wajibu wake ili sote kwa umoja wetu tuilinde Chato yetu, ameongeza kwa kusema, "haipendezi mwananchi unakaa eneo lako ni chafu lakini unasubiria Mkuu wa wilaya na Timu yake au Mkurugenzi waje wakwambia eneo lako chafu ndo ufanye usafi"

Matangazo

  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA CHATO WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI MAENEO YA BIASHARA STENDI MPYA KAHUMO January 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2022
  • View All

Habari Mpya

  • "NENDENI MKAWASAIDIE WAKULIMA WALIME KILIMO CHENYE TIJA WAACHANE NA KILIMO CHA MAZOEA" DC CHATO

    March 21, 2023
  • STENDI YA CHATO INAFANYA KAZI ACHENI UPOTOSHAJI

    March 16, 2023
  • SHAMLA SHAMLA ZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KATIKA HALMASHAURI YA CHATO ZAPAMBWA NA UTOAJI WA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 107 KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    March 08, 2023
  • "NENDENI MKATUMIE PIKIPIKI HIZI KWA KAZI ZA SERIKALI NASI VINGINEVYO" DED CHATO

    March 02, 2023
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.