• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA – CHATO NI NZURI TUITANGAZE

Posted on: January 15th, 2022


Kamati ya siasa ya mkoa wa Geita imepongeza uamuzi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuamua kujenga hospitali ya rufaa ya kanda iliyopo Chato na wameshauri jitihada mbalimbali za kuitangaza hospitali hiyo zifanyike ili wananchi waweze kuifahamu na kwenda kupata huduma za matibabu hospitalini hapo.

Hayo yamesemwa leo tarehe 15 Januari 2022 na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wa Geita ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Mhe. Said Kalidushi na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule wakati wa ziara ya siku moja ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM wilayani hapa.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Mhe. Said Kalidushi amesema kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali katika hospitali hiyo ni muda muafaka sasa wa wananchi uifahamu  na kufika hospitalini hapo ili kuweza kupatiwa huduma mbalimbali za matibabu  badala ya kwenda nje ya nchi ambapo hospitali hiyo hivi sasa imeanza kutoa matibabu kwa wagojwa wa nje.

"Hebu tuitangaze hospitali hii wananchi wote wajue ikoje, hospitali kwa sasa ipo vizuri sana si lazima sana uende hospitali zingine wakati hapa kuna huduma nzuri tena ambazo zamani tulizifuata nje ya nchi" alisema mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita  Mhe. Rosemary Senyamule amesema  kazi nzuri  inayofanywa katika katika hospitali hiyo ni kutokana na serikali kutoa fedha kwa wakati ambapo pia amewapongeza wakala wa majengo Tanzania (TBA) kwa kusimamia vyema ujenzi huo.

Wakikagua kikundi cha bodaboda kikichopo Mpogoloni mjini Chato Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita ndugu Said Kalidushi amesema vijana wengi wamekuwa wakipewa mikopo lakini wamekuwa hawajiwekei malengo kutokana na wengi wao kukata tamaa na kudharau kazi ndogo ndogo wanazofanya hivyo amewaasa vijana hao kufanya kazi kwa kujiwekea malengo ili waweze kufikia ndoto zao.

"Nataka niwaambie hizi biashara mnazofanya jiwekeeni malengo ya baadae maana umri unaenda, tumieni vikao mjadiliane namna ya kuboresha maisha yenu ili mfanye mambo makubwa zaidi, mnaweza fikiria kukopa gari badala ya hizi bodaboda mlizo nazo hivi sasa"  alisisisitiza mwenyekiti wa CCM mkoa.

Awali wakikagua miradi ya ujenzi wa madarasa yaliyojengwa kutokana mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya uviko 19 katika shule shikizi ya Mkombozi na Sekondari ya Buhingo Chato kamati hiyo imeipongeza uongozi wa Wilaya ya Chato kwa usimamizi mzuri na imeagiza kukamilisha kasoro ndogondogo zilizopo ili wanafunzi watakapofungua shule madarasa hayo yaweze kutumika.

Miradi mingine ambayo imekaguliwa ni pamoja na ujenzi wa barabara ya lami Ntarambe  km 2 iliyopo Muungano ambayo imegharimu shilingi 1,007,132,000.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.