• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA CHATO YAKOSHWA NA MIRADI YA MAJI

Posted on: November 9th, 2022

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Chato leo imekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) ambapo wamepongeza jitihada za Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kusogeza huduma za maji karibu na wananchi.


Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe Martha Mkupasi amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi za miradi ya maji Wilayani Chato ambapo amesema miradi mingi ya maji imeweza kutekelezwa kwa kipindi cha muda mfupi  hivyo amewataka wananchi kuhakikisha wanailinda miundombinu ya maji iliyopo katika maeneo yao ili kuepuka uharibifu wa miundombinu hiyo "Tunamshukuru sana mheshimiwa Rais Samia kwa fedha nyingi kwenye miradi ya maji, kazi yetu hapani ni kuendelea kuilinda miundombinu hii ili maji yaendelee kutokana muda wote" amesema Mkuu wa Wilaya.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato ndugu Mandia Kihiyo amesema hapo awali kulikuwa na tatizo kubwa la uapatikanaji wa maji katika kata ya Kachwamba hususani kwenye kituo cha afya cha Kachwamba ambapo amesema kupitia mradi wa maji wa Imalabupina Ichwankima tayari maji yamefika kata ya Kachwamba hivyo ameshauri RUWASA kuhakikisha huduma ya maji inafika katika taasisi zote zilizopo wilayani hapa.


Mkurugenzi Mtendaji pia amesema mwezi Oktoba na Novemba 2022 katika kata ya Kachwamba pekee, serikali ya awamu ya sita imeleta fedha kiasi cha shilingi milioni 400 za kujenga shule mpya msingi Ipandikilo na shilingi milioni 60 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa matatu katika shule ya Sekondari Buhingo-Chato.


Diwani wa kata ya Ilemela Mhe. fortunatus Jangole emesema kukamilika kwa mradi wa maji wa Nyambogo Ilemela ni jambo la faraja kubwa kwa wananchi hao, hivyo amewataka wananchi wa kata ya Ilemela kuitunza vyema miundonbinu hiyo.


Diwani wa kata ya Kachwamba mhe. Stela Masabile amesema kupatikana maji katika kata hiyo kutasaidia kupunguza adha kubwa ya maji ambayo imekuwa ni tatizo sugu na la muda mrefu kwa wananchi hao.


Naye diwani wa kata ya Muganza mhe. Emmanuel Nyamuranga amesema kukamilika kwa miradi wa maji wa Muganza kutapunguza tatizo la maji kwa wananchi wapatao elfu 30 wa kata hiyo hivyo amemshukuru mhe Rais kwa kuweza kuwakumbuka wananchi wa Muganza.


Meneja wa RUWASA Wilaya ya Chato mhandisi Avitus Exavery amesema kwa sasa miradi ya maji ya Nyambogo Ilemela, na Kachwamba imeshakamilika na imeanza kutoa huduma ambapo mradi wa Muganza Bwongera unaendelea kutekelezwa ambapo umefikia asilimia  95 na unatarajiwa kukamilika mnamo tarehe 30 Januari 2023.


Miradi iliyotembelewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ni pamoja na mradi wa maji wa Nyambongo Ilemela, Kachwamba na Muganza Bwongera

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • DC BURA AKABIDHI PIKIPIKI 8 KWA MAAFISA MIFUGO

    June 24, 2025
  • CMT YATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 1.9

    May 29, 2025
  • NENDENI MKATANGAZE MIRADI NA SHUGHULI ZINAZOFANYWA SERIKALI, MHE. MCHENGELWA

    May 23, 2025
  • MAKAMPUNI 12 KUNUNUA ZAO LA PAMBA CHATO

    May 15, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.