• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

MAAFISA AFYA WAJENGEWA UWEZO KUPATA JAMII YENYE AFYA BORA

Posted on: September 17th, 2025


Mkuu wa kitengo cha udhibiti taka na usafi wa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Bi. Fransisca Charles aliongoza kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa kampeni ya mazingira pamoja na kuwapitisha wajumbe wa kikao kwenye takwimu za usafi wa mazingira ambapo kilihusisha maafisa afya wote waliopo katika Halmashauri hiyo.

Kikao hicho kilifanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Septemba 15 hadi 16, 2025 katika ukumbi mdogo wa mikutano uliopo jengo la Uthibiti Ubora wa Shule lililopo karibu na jengo la Halmashauri hiyo ambapo kila Afisa afya aliwasilisha taarifa za utekelezaji wa majukumu yake.

Bi. Fransisca aliwataka maafisa afya hao kuzingatia usafi wa mazingira unaotengeneza soko (MBS) ikihusisha upatikanaji wa huduma kwa wote  hususani katika suala la vifaa vya ujenzi wa vyoo bora vijijini, kutokana na mbinu hiyo kusaidia jamii kupanda kiwango cha usafi pamoja na kupunguza jamii kurudi nyuma hata baada ya majanga ya mafuriko.

"Maafisa afya wenzangu nawapongeza sana kwa kazi nzuri mnayoifanya hususani kazi kubwa mliyoifanya wakati wa maandalizi ya ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025 wilayani kwetu,  nawakumbusha pia kuendelea kuifanyia kazi kikamilifu kauli mbiu yetu isemayo" Mtu ni afya" ambayo inajipambanua katika  maeneo ya ujenzi bora wa vyoo, unawaji mikono, hedhi salama, usafishaji wa mazingira, lishe, udhibiti taka pamoja na ufanyaji wa mazoezi, pia tuzingatie kutumia Community Led Total Sanitation (CLTS) wakati wa ukaguzi wetu kwenye kaya maana kwa kufanya hivyo tutakuwa tunaitendea haki taaluma yetu na tutapata mazingira safi lakini pia tunatengeneza jamii yenye afya bora." Alisema Bi Fransisca

Pamoja na kujadili hali ya utekelezaji wa majukumu pia kikao hicho kiliweka maazimio ambayo kila mmoja alitakiwa kwenda kuyatekeleza kwa ufasaha ambayo ni ukaguzi wa chumvi zinazouzwa madukani na Sokoni kuzia kuuzwa chumvi zisizo na madini joto, kudhibiti uuzaji holela wa vyakula, kufuatilia uwepo wa vyoo bora kwenye Ofisi za taasisi hususani shule na vituo vya kutolea huduma za afya ili ziwe mfano wa kuigwa na jamii, kuzingatia uhakiki wa takwimu za kaya wanazohudumia, kukusanya mapato ya kitengo husika na halmashauri kwa ujumla.

Halmashauri ya wilaya ya Chato ina jumla ya Kaya 70,697 kutoka kata 23 na vijiji 115, ambazo zinahudumiwa na maafisa afya 06 na 02 kutoka makao makuu ya wilaya hiyo wanaohakikisha jamii inakuwa katika hali ya usafi na kupata afya njema ili waweze kuendelea kutekeleza majukumu yao pamoja na ya Serikali kikamilifu.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI YA HUDUMA YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA VIKUNDI

    October 01, 2025
  • DC BURA AFUNGUA ZAHANATI YA NYARUTUTU

    September 30, 2025
  • MHE. BURA AAGIZA UWEZESHAJI KWA WAJASIRIAMALI ILI KUSHINDANA KIMATAIFA

    September 25, 2025
  • KAMISHNA TUME HURU YA UCHAGUZI AKAGUA MAANDALIZI YA UCHAGUZI - CHATO

    September 22, 2025
  • View All

Video

MAANDALIZI YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025 WILAYANI CHATO
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.