Mhe. George Simbachawene waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, amewapongeza viongozi wa wilaya ya Chato Kwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo unaopelekea kuwa na ubora wenye viwango vya juu.
Akiwa katika ziar8a ya kikazi ya siku moja Mhe. Simbachawene amepata fursa ya kutembelea na kukagua Miradi mbalimbali inayotekelezwa ndani ya Halmashauri kupitia Mfuko wa TASAF, na baada kuongea na Watumishi wa Umma katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri
Licha ya kuongea na watumishi Mhe. Simbachawene ametoa pongezi kwa Menejimenti pamoja na watumishi wote mapema hii Leo Septemba 14, 2023 katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya, wakati akizungumza na watumishi wa Umma wa wilaya hiyo, ikiwa ni baada ya kukamilisha ziara aliyoifanya kukagua miradi ya maendeleo hususani miradi iliyo chini ya wizara yake inayotekelezwa na TASAF ambayo ni ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Mkungo na kituo Cha Afya Nyabilezi yote ikiwa kata ya Bukome.
"Nimefurahishwa saana na ninawapongeza viongozi Kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo hususani mradi wa kituo Cha Afya Nyabilezi majengo yake ni imara na yanavutia niwasihi muyatunze Kwa kuzingatia usafi Ili yaweze kudumu" Alisema Simbachawene.
Aidha amewashauri watumishi wa Umma kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha Kwa kile wanachokipata, itakayowapelekea kuwa na makazi bora pamoja na kujiwekeza katika miradi ya maendeleo kuliko kusubiri kiinua mgongo huku wakiwa hawana walichojiandaa.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chato, Mhe. Medard Kalemani ameishukuru Serikali ya awamu ya sita, Kwa jinsi inavyo toa pesa Kwa miradi mingi Kila sekta ukienda afya ipo vizuri Elimu, barabara, umeme na maji.
"Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Daktari Samia Suluhu Hassan ni imara na yenye kujikita kwenye utekelezaji, nawaomba watumishi tusimuangushe Mama yetu ambaye Nia yake kubwa ni kuona wananchi wanapata huduma nzuri hivyo tuchape kazi Kila Mmoja Kwa nafasi yake." Alisema Kalemani
Mhe. Christiani Manunga mwenyekiti wa Halmashauri ya Chato, kupitia kikao hicho Kwa niaba ya Wana Chato amemkabidhi Mhe. Waziri Simbachawene kiwanja ambacho amemuomba kukijenga ili naye awe mwanafamilia wa Chato, jambo ambalo Waziri amelipokea vizuri kuahidi atatekelez
MKURUGENZI MTENDAJI
Postal Address: 116 CHATO
Telephone: +255282228007
Mobile:
Barua pepe: ded@chatodc.go.tz
Copyright©2016 CDC . All rights reserved.