• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

RAIS KENYATA AKEMEA KAULI ZA KICHOCHEZI

Posted on: July 5th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Muigai Kenyatta ameonya tabia ya baadhi ya watu wanaotoa kauli za uchochezi unaolenga kudhohofisha uhusiano wa kirafiki, kidugu na kijirani uliopo kati ya Kenya na Tanzania na amebainisha kuwa vitendo hivyo haviwezi kuruhusiwa kuwagawa Wakenya na Watanzania.

Mhe. Rais Kenyatta amesema leo wakati akiwasalimu wananchi muda mfupi baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita katika siku ya kwanza ya ziara yake binafsi ya kumtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliyepo mapumzikoni Chato Mkoani Geita.

Amefafanua kuwa Tanzania na Kenya zimejaaliwa kuwa na mali nyingi, kuongea lugha moja ya Kiswahili na wananchi wake wanashirikiana kwa mambo mengi, hivyo kauli ama vitendo vyovyote vinavyolenga kuharibu uhusiano huu mzuri havikubaliki na havitafanikiwa.
“Nimekuja hapa Chato kama ndugu, jirani na rafiki. Na hii ndio Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo sisi tunataka, sio jumuiya ya watu ambao wana fikira ndogo, za zamani, za kikabila, za ujinga, sisi tunataka jumuiya ya watu wenye maono ya mbele, ambao wanajua kwamba Kenya ikitajirika Tanzania imetajirika, Tanzania ikitajirika Kenya imetajirika, watu ambao hawawagawi watu kwa mambo madogomadogo ambayo hayasaidii” amesema Mhe. Rais Kenyatta.

Mhe. Rais Kenyatta ameongeza kuwa katika uongozi wake anatamani kuona Jumuiya ya Afrika Mashariki inaungana na kuwa kitu kimoja, wananchi wake wanakuwa huru kwenda nchi yoyote ndani ya jumuiya na ametoa wito kwa wana Afrika Mashariki kujielekeza katika kuzijenga nchi zao kimaendeleo badala ya kupoteza muda mwingi kwa porojo za kisiasa.

Amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa juhudi kubwa anazizofanya kujenga uchumi wa Watanzania na pia amepongeza ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato ambao amesema utasaidia kukuza biashara, ujenzi wa viwanda na uwekezaji mwingine katika eneo hilo na nchi jirani.
Kwa upande wake, Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Rais Kenyatta kwa kuomba kuja kumtembelea akiwa mapumzikoni Chato, na amebainisha kuwa ziara yake ni uthibitisho kuwa uhusiano wa Tanzania na Kenya ni mzuri na Wakenya na Watanzania ni wamoja.
Mhe. Rais Magufuli amefafanua kuwa uhusiano wa Tanzania na Kenya umeanza kabla ya uhuru ambapo Watanzania wanaona Kenya ni nyumbani kwao na Wakenya wanaona Tanzania ni nyumbani kwao, na kwamba nchi hizo zimekuwa zikishirikiana katika maeneo mengi ya kiuchumi, kijamii na kitamaduni.

Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Kenyatta kwa kukemea na kuchukua hatua dhidi ya kiongozi mmoja wa siasa nchini Kenya aliyetoa kauli za kichochezi zilizolenga kuharibu uhusiano mzuri wa Watanzania na Wakenya na amemhakikishia kuwa Watanzania wanawapenda Wakenya.
Amesisitiza kuwa Tanzania na Kenya zinashirikiana katika miradi mingi ikiwemo ujenzi wa miundombinu kama vile barabara ya Arusha – Namanga – Arthi River nchini Kenya, vituo vya huduma za pamoja vya mipaka ya Holili na Namanga, na hivi sasa mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha – Holili – Taveta, mradi wa kusafirisha umeme kutoka Tanzania kwenda Kenya na maandalizi yanaendelea ya kujenga barabara ya lami ya Bagamoyo (Tanzania) – Mombasa (Kenya).

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.