Kamati ya ufuatiliaji wa miradi na tathmini ya Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Novemba 06, 2025 ilifanya ziara ya kukagua ujenzi wa majosho 15 ya kuogeshea mifugo, Ukarabati wa machinjio 02 ambayo ni ya Muganza na kata ya Muungano , ujenzi wa shule ya awali na msingi Nyabugera Kata ya Mganza pamoja na ufuatiliaji wa ujenzi wa bwalo la chakula shule ya Sekondari Zakia Meghji iliyopo kata ya Muganza .
Timu hiyo iliyoongozwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg. Geriad Mgoba ambaye ni Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, ilitembelea na kukagua Miradi yenye thamani ya Tsh.746,271,428.4 ambayo ni majosho 15 yenye thamani ya Tsh. 428,571,428.4 ambapo kila moja limegharimu Tsh. 28,571,428.56, Ukarabati wa machinjio 02 Tsh. 10,000,000/=( Mapato ya ndani), kila moja Tsh. 5.000.000, Bwalo la chakula Zakia Meghji Sekondari 100,000,000/= pamoja na ujenzi wa Shule ya awali na Msingi Juhudi Tsh. 207,700,000/=.(Serikali Kuu)
Licha ya kuipongeza Serikali kwa utekelezaji wa miradi katika kila Sekta, Ndg.Mgoba alisema uwepo wa majosho hayo utapunguza kwa kiwango kikubwa magonjwa ya ngozi kwa mifugo,magonjwa yatokanayo na Kupe hivyo mifugo kuwa na afya njema na kupelekea mazao yatokanayo na mifugo hiyo kuwa na ubora hivyo mfugaji kunufaika na Soko la uhakika ndani na nje ya nchi.Mfugaji wa Ng'ombe wa kata ya Bukome kijiji cha Nyabilezi Ndg.Juma Subhi akizungumza kwa niaba ya wafugaji ameishukuru Serikali kwa kuwasogezea huduma ya josho, ambapo amekiri kuwa awali walikuwa wanafuata huduma ya kuogesha mifugo umbali wa kilometa 20 lakini kwa sasa huduma imesogezwa hivyo Josho hilo litakapokamilika na kuanza kulitumia watanufaika kwa kupata huduma karibu na kuboresha afya ya mifugo yao hivyo kukuza uchumi wa familia na Taifa kutokana na Soko kuwa zuri zaidi.
Halmashauri ya wilaya ya Chato ilipokea fedha za ujenzi wa majosho15 kwa mwaka wa fedha 2025/ 26fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo wa Kunusuru kaya Masikini (TASAF)ambayo yanajengwa katika kata za Makurugusi,Bwera, Muganza,Buseresere,Ilemela,Nyamirembe,Kigongo, Bwina,Iparamasa,Nyarutembo,Katende,Ilyamchele,Kachwamba na Bukome
MKURUGENZI MTENDAJI
Postal Address: 116 CHATO
Telephone: +255282228007
Mobile:
Barua pepe: ded@chatodc.go.tz
Copyright©2016 CDC . All rights reserved.