• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

WANUFAIKA WA TASAF CHATO WAIBUKIA KWENYE UFUGAJI

Posted on: November 21st, 2018

Bibi Sigwa Bushuwandama mkazi wa kijiji cha Mkungo kata ya Bukome kupitia mpango wa TASAF 3 ameanzisha ufugaji wa Mbuzi na Kondoo kama njia mojawapo ya kujiongezea kipato cha familia yake yenye watoto watano


Bwana Mapinduzi Elkana (kulia) baada ya kuanza kunufaika na mpango wa TASAF 3 aliamua kuchimba kisima na kuanza kuuza maji kwa wakazi wa kijiji cha Mkungo ambapo kwa siku anakadiria kuuza ndoo 40 sawa na shilingi 4000 kwa siku

Bibi Tekla Mashine mkazi wa kijiji cha Kanyama kata ya Ilemela baada ya kuanza kunufaika na mpango wa TASAF 3 alianza kufuga mbuzi mradi ambao umemwezesha kuweka umeme wa jua kwenye nyumba yake na kupeleka watoto 6 shule ya msingi na sekondari


Bibi Nyamarwa Justine mkazi wa kijiji cha Kanyama kata ya Ilemela Wilayani Chato mbali na ufugaji wa mbuzi ameweza kujenga nyumba ya vyumba vitatu na matarajio yake ni kukamilisha ujenzi huo mwaka 2019.

Bi Maria Jacob mkazi wa kijiji cha Nyang’omango kupitia mpango wa TASAF 3 ameweza kununua vyombo vyua kisasa kwa ajili ya matumizi ya familia yake.


Baadhi ya wanufaika wa mpango wa TASAF awamu ya tatu Wilayani wameendelea kujiongezea kipato kwa kufuga aina mbalimbali za mifugo.

Baadhi ya wanufaika wamesema kupitia ufugaji wameona ndio njia pekee ya kwao kujikwamua na hali ngumu ya maisha ambayo walikuwa nayo kabla ya kuingia kwenye mpango wa TASAF 3 wa kunusuru kaya masikini.

Bi Sugwa Bushuwandama mkazi wa kijiji cha Mkungo kata ya Bukome Wilayani hapa anasema kupitia mpango wa TASAF 3 kwa kipato kidogo anachopata hivi sasa anao mbuzi 12 ambao mara kwa mara amekuwa anauza na kununua mahitaji mengine ya familia kama vile chakula.

“mwezi uliopita niliuza mbuzi wawili nilienda kufanya manunuzi mnadani ambapo nilinunua gunia la mahindi la shilingi elfu 40 na nguo za wanangu” alisema Bi Sugwa huku akitabasamu.

Kwa upande mwingine wanufaika hao wanasema kupitia miradi ya ufugaji wa Ng’ombe na mbuzi kwao imekuwa ni rahisi kutokana na urahisi pindi wanapotaka kuuza au kubadili kupata bidhaa nyingine kama vile chakula pindi familia zinapokuwa kwenye ukata.

Bi Lega Amos mkazi wa kijiji cha Nyambiti kata ya Nyamirembe ambaye ana mbuzi 17 amesema baada ya kuanza kunufaika na mpango wa TASAF 3 alianza kununua mbuzi wawili lakini hadi sasa kupitia ufugaji huo ameanzisha mradi wa kukaanga samaki na kuuza kwenye soko la kijijini hapo lakini pia ameweza kujenga nyumba ndogo ya tofali za tope na kuezeka kwa bati.

“sasa hivi naweza kulisha, kuvalisha na hata kusomesha hawa watoto ambao wote ninawalea, Nina nyumba ya bati lakini pia ninaishi vizuri na familia yangu” alisema Bi Lega.

Kwa ujumla wanufaika wengi wa mpango wa TASAF 3 Wilayani Chato wamejikita zaidi kwenye ufugaji wa Mbuzi na Ng’ombe ambao kwao wanasema huleta matokeo ya haraka wakati familia ikiwa kwenye wakati mgumu wa kiuchumi.

Kupitia miradi hiyo ya ufugaji wanufaika hao wameomba kutembelewa na wataalamu wa mifugo kwa ajili ya ushauri wa ufugaji bora pamoja na utengenezaji wa mabanda imara kwa ajili ya mifugo yao.

Wilaya ya Chato ina jumla ya wanufaika wa TASAF awamu ya tatu 7,666 Kati yao wanufaika 1000 Wamejikita kwenye miradi ya ufugaji wa mbuzi na Ng’ombe na baadhi wameanzisha biashara ndogo ndogo kama njia ya kujiongezea kipato cha kaya.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.