• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

WAZIRI JAFO AWAONYA WATUMISHI WAZEMBE CHATO

Posted on: October 20th, 2018

Waziri Jafo akikagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni kwa ajili ya kuanza kwa kidato cha tano na sita shule ya sekondari Bwina iliyopo Chato

Baadhi watumishi wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wakimsikiliza Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo la Chato Mhe. Dkt. Medard Kalemani

Waziri wa nchi ofisi ya Rais- TAMISEMI Selemani Jafo akiongea na watumishi wa Halmashauri kwnye ukumbi wa mikutano


Waziri wa nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Selemani Jafo amesema watumishi wazembe waliopo Halmashauri ya Wilaya ya Chato hasa wakuu wa idara wabadilike kuanzia sasa na si kuhamishwa vituo vya kazi.

Waziri Jafo amesema hayo leo  wakati akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya Chato  kwenye ziara yake ya siku moja Wilayani hapa.

”Wakuu wa idara fanyeni kazi, saidianeni, fanyeni kazi kama timu, ondoeni ubinafsi katika kazi ili kuleta mabadiliko hapa Chato… lakini wale watakaoshindwa kujirekebisha kuanzia leo hatutawahamisha bali tutawashusha vyeo mara moja” amesema Waziri Jafo.

Waziri Jafo amesema kutokana na mabadiliko ya viongozi yaliyotokea Wilayani Chato, anatarajia shughuli mbalimbali zitatekelezwa vizuri na kwa wakati ambapo amewataka watumishi kuwapa ushirikiano viongozi hao.

Waziri Jafo pia amewataka wakuu wa idara katika maeneo mbalimbali nchini kufanya kazi zao kwa kujiamini na kuacha kushinikizwa na wanasiasa ambao wamekuwa chanzo cha kuvuruga shughuli mbalimbali hususan fedha zinazopelekwa  kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Waziri Jafo katika ziara yake ametembelea shule ya Sekondari Buseresere ambapo amesema serikali italeta fedha shuleni hapo kiasi cha Shilingi milioni 250 kwa ajili ya uanzishaji wa kidato cha tano na sita shuleni hapo na amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chato Eliurd Mwaiteleke kuhakikisha ujenzi huo unakamilika ifikapo Februari 2019.

Maeneo mengine yaliyotembelewa na Waziri Jafo ni pamoja na Ujenzi wa sekondari ya Minkoto, Zahanati ya Mutundu ambayo ameagiza utaratibu wa kuipandisha hadhi na kuwa kituo cha Afya uanze, Ujenzi wa sekondari ya kidato cha tano na sita sekondari ya Bwina ambapo pia ameagiza wizara ya elimu kuhakikisha inapeleka wanafunzoi wa kidato cha tano ili shule hiyo iweze kuanza mapema, ujenzi wa sekondari ya Kikumbaitale na Zahanati ya kata ya Ilemela ambayo inapandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya na ujenzi wake utaanza mapema mwezi huu.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.