• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

ZAHANATI YA NYARUTUTU MBIONI KUANZA KAZI

Posted on: September 16th, 2025


Mganga mkuu Dr Daniel Mzee, ameongoza kikao cha maandalizi ya Ufunguzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nyarututu kilichopo Kata ya Bwanga. Akiongoza kikao hicho Dr Mzee amewapongeza uongozi wa Kijiji,wajumbe wa halmashauri ya kijiji kwa ushirikiani mkubwa waliotoa tangu ujenzi ulipoanza hadi kituo kilivokamilika. “Tunaishukuru Serikali kupitia TASAF (Mfuko wa Maendeleo ya Jamii) kwa kuhakikisha kijiji cha Nyarututu kinasogezewa karibu huduma za Afya kwa Kufadhili Ujenzi wa Zahanati na kuwaepushia adha ya kusafiri kufata huduma mbali. Pia tunawapongeza sana wana kijiji pamoja na uongozi wenu kwa kujitoa na kutoa ushirikiano wa kutosha hadi Zahanati imekamilika”.

Dr Mzee aliwajulisha wajumbe wa kikao kuwa usajili wa Zahanati umekamilika na tayari imeshapatiwa watumishi watatu ambao ni Mganga Mfawidhi na wauguzi wawili, hivyo Zahanati inapaswa kuanza kazi na kuwaomba halmashauri ya kijiji kuhakikisha vifaa vya matumizi ya ofisi vinapatikana kwa nguvu za wana kijiji.Vifaa hivyo ni Mabenchi ya kukalia wagonjwa 10, Meza 8, Viti 16, Kabati la kuhifadhia  dawa, maji kwa ajili ya matumizi ya zahanati na kupatika mlinzi wa Zahanati.

Mfamasia wa Wilaya Daniel Mbasagule alisisitiza wajumbe juu ya kutoa elimu sahihi kwa wana kijiji juu ya upatikanaji wa huduma katika zahanati ambazo zinapatikana kwa mifumo mitatu.Mfumo wa kwanza ni wa malipo ya papo kwa papo, mfumo wa matibabu ya bure au msamaha ambayo serikali huchangia kwa wajawazito,watoto chini ya miaka mitano,wazee wa miaka 60 na kuendelea,walemavu na watu wenye magonjwa sugu, na mfumo wa matibabu kwa bima ya jamii ICHF.

Akishukuru kwa niaba ya Kijiji,mwenyekiti wa kijiji Ndg.Felecian Chiza amesema wanaishukuru sana Serikali kwa kuwasogezea huduma ya Afya Karibu ambapo awali iliwalazimu kufata huduma umbali wa Km 5 katika kituo cha Afya Bwanga. Mwenyekiti aliahidi ofisi ya Mganga mkuu kuwa wataendelea kutoa ushirikiano wa karibu muda wote na kuhakikisha vifaa vya matumizi ya ofisi vinapatikana ili kituo kianze kufanya kazi kwa wakati na kwa ufanisi.

Ujenzi wa Zahanati ya Nyarututu ulianza mnamo tarehe 22.01.2025 na kukamilika  mwezi Agosti 2025 na kutumia jumla ya Tsh 92,410,714.29 fedha kutoka Serikali kuu (TASAF) na Tsh 7,700,000.00 nguvu za wananchi. Zahanati ilizinduliwa rasmi na Ndg. Ismail Ali Ussi kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa zilizofanyika tarehe 06.09.2025 katika Wilaya ya Chato.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • ZAHANATI YA NYARUTUTU MBIONI KUANZA KAZI

    September 16, 2025
  • DC BURA AZINDUA KAMPENI YA CHANJO NA UTAMBUZI MIFUGO

    September 11, 2025
  • CMT YAFANYA ZIARA KUKAGUA UKAMILISHWAJI WA MIRADI YA MAJOSHO

    August 28, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAPEWA MAELEKEZO MAALUMU KAMPENI YA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU YA NG'OMBE

    August 28, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.