• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

SEKTA YA KILIMO NA UMWAGILIAJI

SEKTA YA KILIMO

Eneo linalofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali ya Chakula na Biashara  ni  jumla ya Hekta 267,900 ambapo hekta zinazolimwa kwa sasa ni  99,123 sawa na asilimia 37.

Mazao Makuu ya Chakula yanayolimwa Wilayani Chato ni Mahindi, Mpunga, Mtama, Mihogo, Maharage na viazi vitamu. Mazao haya pia hutumika kama Mazao ya Biashara. Mazao Makuu ya Biashara ni Pamba, Tumbaku na Alizeti.

Mkakati wa Wilaya katika kuendeleza  sekta ya kilimo kwa kuzingatia Mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa na Mapinduzi ya kijani ni kuhakikisha uwepo wa “Uhakika wa Chakula  na Ongezeko la Kipato Ngazi ya Kaya”.

 UZALISHAJI WA MAZAO MSIMU WA 2016/2017

Katika msimu wa Kilimo wa 2016/2017, Wilaya ya Chato ililenga kulima jumla ya Hekta

71,267 za mazao ya chakula ambapo tulitarajia kuzalisha tani 298,696 na hivyo kuwa na ziada ya tani 174,658. Jumla ya Hekta 36,577 za mazao ya chakula zililimwa, sawa na 51% ya malengo, ambapo mavuno yote ni Tani 53,019 (wanga 47,962 na protini 5,057) sawa na asilimia 18% ya malengo. Baada ya kutoa maganda/makapi, chakula halisi ni tani 32,978 (wanga tani 27,921 na protini tani 5,057).

Wilaya ya Chato inakadiriwa kuwa na watu 420,191 (kwa mujibu wa taarifa ya NBS mwaka 2017), na mahitaji yake ya chakula kwa mwaka 2017/2018 ni tani 88,071 za wanga na tani 35,967 za protini.

MALENGO YA KILIMO NA UTEKELEZAJI MSIMU WA 2017/2018

Katika msimu huu wa kilimo Wilaya imelenga kuzalisha jumla ya Tani 245,520 za mazao ya chakula sawa na kulima hekta 65,194.4 uhamasishaji unaendelea. Kwa Upande wa mazao ya Biashara malengo ni kuzalisha tani 16,904 sawa na kulima hekta 14,195.2.

 

SEKTA YA UMWAGILIAJI

Eneo linalofaa kwa kilimo cha Umwagiliaji ambalo ni hekta 10,810 na kuanza uendelezaji wake ambapo hadi sasa hekta zinazomwagiliwa kwa njia mbalimbali ni 3416 sawa na asilimia 31.6% ya eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji.

Mkakati mkubwa wa Wilaya kwa sasa ni ujenzi wa skimu kubwa na ndogo ili kuongeza eneo linalomwagiliwa ambapo kwa sasa ujenzi wa skimu ya umwagiliaji katika kijiji cha Nyisanzi kupitia Mpango wa kilimo wa Wilaya (DADP) kwa thamani ya Tshs. 881,557,416.40 umesimama kutokana na uhaba wa fedha ambayo ikikamilika itaweza kumwagilia hekta 250 na kuongeza eneo la umwagiliaji hadi kufikia hekta 3666. Mradi huu unatekelezwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji lakini hata hivyo ni kwa muda mrefu sasa Mradi huu umesimama licha ya juhudi za uongozi wa Wilaya kufuatilia Wizarani.

Aidha tumetekeleza Mradi mmoja katika kijiji cha Kibehe, kitongoji cha Masasi Kwa kuchimba kisima kirefu Kwa ufadhili wa shirika la Tumaini Fund. Kwa sasa Shirika la Tumaini Fund limeanza upanuzi wa mradi wa kutoa maji ziwa Victoria kwa umbali wa kilomita 4 ambao utakua na uwezo wa kumwagilia Hekta 75 sawa na Ekari 187.5

 

Katika juhudi za kuendeleza kilimo cha umwagiliaji Wilaya ya Chato, timu ya umwagiliaji wilaya kushirikiana na Timu ya kanda (Zonal Irrigation Office) tulifanya utambuzi (Reconnaissances) wa maeneo/mabonde muhimu (Nyamirembe-Masasi, Kibumba, na Makurugusi) kwa ajili ya kuendelezwa kwa ajili ya miradi ya umwagiliaji ilifanyika na mapendekezo ya Timu hiyo yalihitaji Wilaya (Kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji) kutafta fedha kiasi cha tsh.500 millioni kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu.

UJENZI WA MRADI WA UMWAGILIAJI KATIKA KIJIJI CHA NYISANZI

Mradi huu unajengwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ukifadhiliwa na mradi wa DASIP na mfuko wa maendeleo ya umwagiliaji wilayani (DIDF). Mkataba wa mradi huu ulisainiwa na ofisi ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika tarehe 24/05/2013 baina ya wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na Mkandarasi kampuni ya NYAKILANG’ANI CONSTRUCTION LTD ya Musoma kwa kutekelezwa ndani ya siku 270 akisimamiwa na mhandisi mshauri ambaye ni kampuni ya CODA Consulting company and Partners ya nchini Kenya kwa thamani ya Tshs. 881,557,416.40. Utekelezaji wa mradi huu ulianza kwa kusuasua na mkataba wake umemalizika tangu 06/02/2014.

 Mpaka sasa utekelezaji wa mradi huu bado haujakamilika, utekelezaji umesimama na wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi haijatoa mwongozo wowote licha ya kuandikia barua tatu kwa wakati tofauti.

Mradi huu ukikamilika utakuwa na uwezo wa kuhudumia hekta 250 za kilimo cha umwagiliaji ambapo zaidi ya wakulima 150 watanufaika.

Hali Halisi ya Ujenzi wa Mradi Hadi Sasa

Hadi sasa kazi iliyofanyika ni ujenzi wa tuta refu lenye urefu wa mita 470 yaani Earth embarkment na sehemu ya kutoroshea maji (spillway) ndio zimejengwa hata hivyo spillway haijajengewa na mawe ili kukazia isije ikageuka kuwa korongo. Aidha miundombinu mingine haijajengwa kama ilivyopangwa kwenye usanifu (design). Miundombinu hiyo ni ujenzi wa mitaro mikuu na midogo sambamba na vigawa maji/mabanio (Diversion boxes), kuweka mipaka na vitoa maji Bwawani (outlets), Upandaji wa nyasi  downstream kwenye tuta hii ni pamoja na upangaji wa mawe upande wa juu wa tuta (upstream) na kufanya backfill ya borrowpit za vifusi.


CHANGAMOTO KATIKA SEKTA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

  • Idadi ndogo ya watumishi ukilinganisha na ikama. (Kilimo mahitaji ni 150 waliopo ni 77 pungufu 73, Ushirika Mahitaji 9 walipo 5 pungufu 4, Umwagiliaji mahitaji 5 waliopo 1.
  • Bajeti ndogo ya Sekta ukilinganisha na idadi ya watumishi na uhitaji wa huduma za ugani kwa jamii.
  • Uhaba wa vitendea kazi – idara haina gari na upungufu wa pikipiki 16 (Ngazi ya Kata)
  • Mwitikio mdogo wawakulima katika kupokea teknolojia mpya.
  • Shughuli za kilimo kutofanyika kwa wakati kutokana na ukosefu wa fedha kulingana na bajeti ilivyo.

 

HATUA ZINAZOCHUKULIWA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO

  • Kuendelea kuomba kibali cha ajira kila mwaka kwa ajili ya kupunguza pengo kubwa la uhaba wa watumishi.
  • Kuendelea kuomba kupanuniliwa kwa ukomo wa bajeti inayotolewa na serikali kila mwaka ili iendane na ongezeko la watumishi sambamba na uhitaji wa huduma za ugani kwa wakulima na vitendea kazi kwa wataalam.
  • Kutoa elimu na mafunzo kwa wakulima yanayolenga kuboresha shughuli zao za   uzalishajimali.

Matangazo

  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA CHATO WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI MAENEO YA BIASHARA STENDI MPYA KAHUMO January 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2022
  • View All

Habari Mpya

  • "NENDENI MKAWASAIDIE WAKULIMA WALIME KILIMO CHENYE TIJA WAACHANE NA KILIMO CHA MAZOEA" DC CHATO

    March 21, 2023
  • STENDI YA CHATO INAFANYA KAZI ACHENI UPOTOSHAJI

    March 16, 2023
  • SHAMLA SHAMLA ZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KATIKA HALMASHAURI YA CHATO ZAPAMBWA NA UTOAJI WA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 107 KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    March 08, 2023
  • "NENDENI MKATUMIE PIKIPIKI HIZI KWA KAZI ZA SERIKALI NASI VINGINEVYO" DED CHATO

    March 02, 2023
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.