• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

ALAT GEITA YAFURAHISHWA NA USIMAMIZI MAKINI WA MIRADI YA MAENDELEO CHATO

Posted on: April 14th, 2024

Wajumbe wa kamati ya Jumuiya ya Tawala za mikoa (ALAT) Mkoa wa Geita inayoundwa na madiwani 2, Mwenyekiti wa halmashauri pamoja na Mkurugenzi Mtendaji kutoka kila wilaya, wameipongeza halmashauri ya wilaya Chato  kwa namna inavyotekeleza miradi ya maendeleo kwa kuzingatia ubora wenye kiwango cha juu.

Pongezi hizo zimetolewa  leo April 13, 2024 na wajumbe wa kamati hiyo wakiongozwa na mwenyekiti wake Mhe.Vicent Busega Lubaga ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbogwe akiwa ni diwani wa kata ya Nhomolwa walipotembelea ujenzi wa soko la samaki linalojengwa kijiji cha Chato kata ya Chato pamoja na ujenzi wa zahanati ya kijiji cha mlimani kata ya Muungano wilayani hapa.

Ujenzi wa zahanati ya kijiji cha mlimani umegharimu kiasi cha Tsh.106,000,000/= (milioni mia moja na sita tu) mpaka kukamilika  kwa mchanganuo wa 32,000,000/= nguvu za wananchi, 24,000,000/= kutoka kwa wadau wa maendeleo na 50,000,000/= kutoka Serikali kuu, zahanati tayari imekamilika na inatoa huduma kwa wananchi.

 Walitembelea pia mradi wa ujenzi wa Soko la Samaki lenye vizimba 24 uliopo kijiji cha Chato kata ya Chato ambao utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.7 (bilioni moja na milioni mia saba tu) fedha kutoka Serikali kuu kupitia wizara ya mifugo na uvuvi na mkandarasi wa mradi ni SHIRIJI CONSTRUCTION LTD huku hatua za ujenzi zikiwa ni 83% na mradi unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi june 2024.

Katika ujenzi wa Soko la Samaki pia kutakuwa na ujenzi wa jengo la kuhifadhia samaki wabichi (Cold room), jengo la kuzalisha barafu (ice room), jengo la utawala, jengo la chanja za umeme za kukaushia dagaa, chanja za nje, jengo la mama lishe lenye vyumba 6, jengo la mlinzi pamoja na jengo la matundu ya vyoo vya ME na KE.

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Chato Mhe. Batholomeo Manunga ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa namna inavyoendelea kuboresha miundo mbinu kila sekta hususani katika wilaya ya Chato ambapo amekiri kuwa wananchi wa Chato wamefarijika na kufurahi mno kwa uwepo wa Soko hili na wanatamani ujenzi ukamilike mapema ili waanze kunufaika  kwa kukuza uchumi wa kaya, wilaya na Taif

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • JIMBO LA CHATO LAGAWANYWA RASMI

    May 12, 2025
  • CHATO TECHNICAL YAPONGEZWA

    May 09, 2025
  • WATAHINIWA 2234 WA KIDATO CHA SITA KUANZA MTIHANI MEI 5 WILAYANI CHATO

    May 04, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 01, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.