• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

BILIONI 2.2 KUBORESHA MIUNDO MBINU YA ELIMU NA AFYA CHATO

Posted on: January 30th, 2025


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Mhe. Christian Manunga, jana Januari 28, 2025 aliambatana na timu ya menejimenti ya halmashauri hiyo katika ziara  ya kutembelea na kukagua ujenzi na  ukamilishaji wa miradi 7 ya Maendeleo ikiwemo ya Elimu na Afya iliyogharimu kiasi cha shilingi 2,227,125,000/= kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025


Miradi iliyotembelewa ni Ujenzi wa madarasa 2 Mwabasabi Sekondari - Iparamasa (50,000,000/=), Upanuzi wa shule kidato cha 5 na 6 Iparamasa Sekondari (918,125,000/=),Shule Mpya ya Sekondari Mwendakulima - Butengorumasa (584,000,000,/=),Bweni la wasichana Butengorumasa Sekondari (138,000,000/=), Ujenzi wa jengo la OPD zahanati ya Kabantange (92,000,000/=), pamoja na ujenzi wa Sekondari Mpya ya Igogo (114,000,000/=) iliyopo kata ya Buziku.


Mhe. Manunga katika ziara hiyo amesisitiza wasimamizi wa miradi kuzingatia sana  nidhamu katika matumizi ya fedha itakayopelekea thamani ya fedha kuonekana kwenye mradi pamoja na kupata majengo yenye ubora ili kutimiza lengo la Serikali  kuwa na miundo mbinu imara itakayowawezesha wahitaji kupata huduma kwenye mazingira mazuri na salama lakini pia kuwapunguzia umbali wanafunzi hususani ukamilishwaji wa shule mpya ya Sekondari  Mwabasabi na Mwendakulima.


"Binafsi namshukuru sana Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutujali wana Chato katika suala zima la miundo mbinu hususani ya elimu na afya, ni jukumu letu kumuunga mkono kwa kutumia vizuri fedha anazotupatia kwa ajili ya miradi, wasimamizi wa miradi zingatieni thamani ya fedha (value for money) usimamizi makini wa fedha sambamba na uimara wa majengo bila kusahau huduma bora kwa wananchi tunaowatumikia ndio shukrani pekee tunayopaswa kuipa Serikali yetu ya awamu ya sita kwa kazi kubwa inayofanya" Alisema Manunga


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwabasabi kata ya Iparamasa Mhe. Justiniani Marco Mtunzile, kwa niaba ya wananchi wake amekiri kufurahishwa na Serikali kuwajengea Shule Mpya ya Sekondari Mwabasabi iliyopo kata ya Iparamasa inayotarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi wa pili 2025, iliyojengwa kwa lengo la kuwapunguzia wanafunzi umbali wa kilometa 16 kwenda shule ya Sekondari Mnekezi wengi wao wakitokea hapo Mwabasabi.


" Serikali imetujali saana, wanafunzi walikuwa wanakwenda umbali wa kilometa 16 na kurudi tena  kilometa 16 kila siku za masomo, lakini kwa sasa watasoma hapahapa Mwabasabi, mimi na wananchi wangu tumekubaliana kuilinda miundo mbinu hii kwa juhudi zote ikiwa ni kuitunza idumu lakini pia kuiunga mkono Serikali yetu sikivu. Alisema Mtunzile


Pamoja na kukagua miradi, pia ziara hiyo ilifanya ufuatiliaji wa kuripoti wanafunzi shuleni mwaka mpya wa masomo 2025 na kubaini kuwa bado kuna wanafunzi wachache hawajaripoti ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Ndg Mandia Kihiyo amewataka watendaji wa kata na vijiji kwa kushirikiana na walimu kuwafuatilia na kuhakikisha wanaripoti shuleni kuendelea na masomo kwani Serikali imefanya kazi kubwa ya kuweka vizuri miundo mbinu  na kufanya mazingira ya kujifunzia kuwa salama na rafiki.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • JIMBO LA CHATO LAGAWANYWA RASMI

    May 12, 2025
  • CHATO TECHNICAL YAPONGEZWA

    May 09, 2025
  • WATAHINIWA 2234 WA KIDATO CHA SITA KUANZA MTIHANI MEI 5 WILAYANI CHATO

    May 04, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 01, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.