• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

BWANGA, MJI WA KIMKAKATI WILAYANI CHATO MKOA WA GEITA

Posted on: September 10th, 2019


Na Richard Bagolele-Chato

Mji wa Bwanga uliopo takribani kilometa 50 kutoka mjini Chato na kilometa 60 kutoka mjini Geita unatajwa kuwa ni moja ya maeneo ambayo yapo kimkakati zaidi kukua na kuwa moja ya miji mikubwa hapa wilayani Chato na mkoani Geita kwa ujumla.

Kwa kuliona hilo kuna baadhi ya mambo ambayo yanatakiwa yaende sambasamba na ukuaji wa mji huo ikiwemo huduma za kijamii na kiuchumi.

Moja wapo ya mambo yaliyomsukuma Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Eliurd Mwaiteleke na badhi ya wakuu wa idara kufika katika mji huo na kufanya mkutano mkubwa na wafanyabiashara kwa lengo la kuboresha soko lililopo mjini hapo.

Mkurugenzi alitoa sababu kuu moja na kubwa ya kwanini soko hilo liendelezwe, kwanza ni mahali ulipo mji wa bwanga ni eneo la kimkakati kutoka na kuwa na njia nne kuu zinazoingia na kutoka mjini hapo ikiwemo ile ya barabara inayoelekea Chato Bukoba, Mtukula na Kampala Uganda, Barabara inayoelekea Biharamulo, Ngara, Rusumo hadi Rwanda, njia inayoelekea Runzewe, Kahama, hadi Dar es Salamaam na ile inayoekelea Geita na Mwanza.

Ukiachilia mbali shughuli za uchimbaji wa madini zinazofanyika katika maeneo mbalimbali ya mji huo, Bwanga ina  kila sababu ya kuwa mji mkubwa wa kiuchumi hivyo basi kwa pamoja na wafanya biashara wamekubaliana kurekebisha soko hilo hili liweze kuwa la kisasa na la kuvutia watumiaji wengi hususan wanaopita barabara kuu kama nilivyotaja hapo juu.

Mkurugenzi ameenda mbali Zaidi na kusema kuna kila sababu ya wafanya biashara hao kufanya biashara hadi usiku ili kutoa huduma kwa wananchi wanaopita katika eneo hilo kama tu miundombinu itaruhusu ikiwemo uwekaji wa taa za barabarani katika mji huo ambapo amesema suala hilo linafanyiwa kazi na kabla ya mwaka 2019 kuisha mji huo utakuwa unanga’ra kwelikweli.

Mji wa Bwanga pia hauna kituo cha mabasi hivyo kufanya wananchi wake wapate shida za hapa na pale lakini Mkurugenzi Mtendaji pia amewatoa hofu wafanyabiashara  hao kwa kusema kuwa kuna mipango kadhaa ya kujenga kituo kikubwa cha mabasi kitakachokuwa kinahudua wananchi hao.

Mkurugenzi Mtendaji pia alieleza pia kuna kila sababu ya kuupima mji huo ili upangike vizuri na watu waweze kujenga kwa kufuata ramani za mipango miji. Suala hili lilitolewa ufafanuzi mzuri na Mkuu wa Idara ya ardhi na Maliasili Deogratias Matiya ambapo amesema idara hiyo iko kwenyue mpango wa kuhamia hapo kwa ajili ya shughuli za upimaji wa mji huo ili uwe wa kisasa Zaidi.

Eneo la uwekezaji wa viwanda katika mji huu pia ni jambo jingine ambalo Mkurugenzi Mtendaji amesema Halmashauri inalifanyia kazi na kuhakikisha eneo hilo la kimkakati linakuwa na viwanda vya kati na vikubwa ukiachilia mbali shughuli za uchimbaji zinazoendelea katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo.

Kuzinduliwa kwa hifadhi mpya ya Burigi Chato kunaufanya mji huu ukue kwa haraka Zaidi kwa watalii wanaotoka nchi za jirani za Uganda, Rwanda na Burundi, hapa kwa makampuni ya kitalii ni sehemu salama na ya kimkakati kuweka ofisi kwani ni  kilometa takrabani 30 kutoka uwanja wa ndege wa Chato lakini mahali hapa utaifikia miji mingine mikubwa iliyopo kanda ya ziwa kama vile Mwanza, Geita, Kahama, Katoro, Buseresere na Bukoba.

Mipango iliyopo hivi sasa ni kuhakikisha mji huo unakuwa na nishati ya umeme ya uhakika ambapo vijiji vyote kwa sasa vina huduma ya umeme kupitia mradi wa REA pamoja na upatikanaji wa huduma ya maji kutoka ziwa Viktoria.

Naiona Bwanga mpya ile inakuja, bila shaka hii ni mipango kabambe kabisa ya kuubadili mji huu unaokadiriwa kuwa na wakazi zaidi ya 33,000 wa maeneo ya Bwanga, Nyakayondwa, Bukirigulu na Izumangabo

Mwandishi wa Makala hii fupi ni Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano  Halmashauri ya Wilaya ya Chato 0755773371

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.