• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

CHATO FAMILY YAIPIGA TAFU CHATO SEKONDARI

Posted on: March 19th, 2018

Umoja wa kikundi cha ‘Whatsap’ cha Chato  Family kimechangia mifuko ya saruji 50 na nondo 12 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa wa sekondari ya Chato.

Akikabidhi vifaa hivyo mmoja ya wanachama wa kundi hilo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro Mhe. Onesmo Buswelu ambaye alihitimu kidato cha nne shuleni hapo mwaka 1996 amesema wameamua kutoa msaada huo ili kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano kwa ujenzi mbalimbali wa miundombinu katika sekta ya elimu ambapo Mheshimiwa Rais Magufuli anajitahidi kuleta maendeleo hivyo ni vyema kumuunga mkono.

“Tunaguswa na kazi za mhe rais... anapambania Taifa hili la Tanzania na Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe na sisi kama sehemu ya watanzania ni vyema tuungane nanyi wanachato” alisema Mhe. Buswelu.

Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa Shule  ya  Sekondari ya Chato Mwalimu Selema Bernado amesema Shule hiyo kwa sasa inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa vinane ambapo kwa sasa kuna vyumba vya madarasa 25 tu ukilinganisha idadi kubwa  ya wanafunzi 1520 waliopo shuleni hapo.

Mwalimu Bernado pia amesema shule hiyo inakabiliwa na Chumba cha Maabara ya Sayansi, ofisi za walimu ambapo husababisha baadhi ya vyumba vya madarasa kutumika kama ofisi ya walimu. Amewashukuru wanakikundi hao kwa msaada huo na kuomba wadau wengine wajitokeze katika kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi shuleni hapo.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji afisa elimu taaluma wa Sekondari Masai Mjule amewashukuru wanakikundi hao kwa mchango wa vifaa hivyo na kusema kuwa upatikanaji wa mchango huo kwa kiasi kikubwa utasaidia kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo.

Chato Family ni kundi la ‘whatsap’ linaloundwa na baadhi wanafunzi waliowahi kusoma sekondari ya Chato na watumishi waliowahi kufanya kazi Wilayani hapa.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.