• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

CMT YAIPONGEZA WATUMISHI FC CHATO KUIBUKA KIDEDEA BONANZA LA WATUMISHI MKOA

Posted on: July 28th, 2025


Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Chato, ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji (W) Ndg Mandia Kihiyo, imeipongeza timu ya mpira wa miguu ya watumishi wa Wilaya hiyo kwa kuibuka kidedea wa Soka katika Bonanza la watumishi wa Mkoa wa Geita lililoandaliwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Martine Shigela na kufanyika Julai 26, 2025.

Pongezi hizo zimetolewa leo Julai 28, 2025 mara baada ya  Afisa utamaduni na Michezo(W) Ndg .Halfan Mbonde (wa kwanza kushoto) aliyeambatana na Nahodha wa timu hiyo Ndg Berino Msigwa kitaaluma ni Afisa Kilimo (wapili kutoka kushoto) walipomkabidhi Mkurugenzi Mtendaji Kombe walilolitwaa katika Bonanza hilo wakati Timu hiyo ya Menejimenti ikiwa katika kikao cha kujadili utendaji kazi wa Halmashauri katika ukumbi wa mikutano wa Wilaya hiyo.

Bonanza hilo lilifanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu iliyopo mkoani humo ambapo michezo mbalimbali ilichezwa ukiwemo Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete, kukimbiza yai kwenye kijiko, kucheza bao, kukimbiza kuku pamoja na mingine mingi ya kuimarisha viungo.

Mbonde Ameeleza kuwa watumishi wa Chato walishiriki michezo ya Mpira wa Miguu, kukimbiza kuku, kukimbia na yai kwenye kijiko, Mashindano ya kula pamoja na mchezo wa bao huku ikipata ushindi katika Soka kumpata golikipa bora ambaye ni Mwl Karim Hamis wa S/Msingi Nyambiti kata ya Nyamirembe na mfungaji bora Mwl Jabiri Mgovano wa  S/Msingi Izenge kata ya Buseresere, wakati kwa upande wa mkimbiza kuku akiibuka mwamba Ndg Frank Ipugute (Afisa Mifugo) na kukimbia na yai akiibuka mshindi wa 3 Ndg Martine Babere mtendaji wa kijiji cha Songambele - Iparamasa.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji Ndg Kihiyo amewapongeza waandaji wa Bonanza lakini pia washiriki wote hususani kutoka Chato kuanzia viongozi wa timu wakiongozwa na Nahodha Ndg Msigwa, wachezaji wa michezo yote  pamoja na washangiliaji kwa kufanikisha kombe kuja Chato ni heshima kubwa na wameiwakilisha vema wilaya, huku akiwataka kujiimarisha zaidi kwa mazoezi kwani wakumbuke Bonanza hilo la watumishi Mkoa wa Geita lilikuwa na lengo la maandalizi ya michuano ya  Shimishumita kitaifa yatakayofanyika mwezi Agosti 2025 Jijini Tanga.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • CMT YAFANYA ZIARA KUKAGUA UKAMILISHWAJI WA MIRADI YA MAJOSHO

    August 28, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAPEWA MAELEKEZO MAALUMU KAMPENI YA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU YA NG'OMBE

    August 28, 2025
  • WATUMISHI WAPYA IDARA YA KILIMO WAPEWA MAFUNDO NA MAZINGATIVU

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UCHUKUAJI FOMU ZA UBUNGE NA UDIWANI LINAENDELEA

    August 26, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.