• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

"HAKIKISHENI KILA MMOJA ANATIMIZA MAJUKUMU YAKE IPASAVYO, DED CHATO"

Posted on: January 22nd, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Chato Ndg. Mandia H. Kihiyo Januari 20/2024 ameendelea na ziara yake ya kata kwa kata shule kwa shule, kutembelea shule zote za Sekondari lengo likiwa ni kufuatilia wanafunzi wa kidato cha kwanza waliopangwa na walioripoti shuleni.


Katika ziara hiyo Ndugu Kihiyo alikutana na timu ya uongozi kuanzia ngazi ya kijiji, Kata, walimu pamoja na wanafunzi ndipo aliwataka kila mmoja atimize majukumu yake kwa uweledi lengo likiwa ni kuhakikisha wanafunzi wote wanaripoti shuleni na walimu kusimamia ufundishaji wenye tija kwa kuzingatia ratiba ya vipindi kwa kadri miongozo inavyowaongoza ili kukuza viwango vya ufaulu.


Aidha aliwataka viongozi hao kuendelea kuwa mfano mzuri katika suala la nidhamu pamoja na kusimamia maadili ya wanafunzi na kuhakikisha wanawalinda dhidi ya vitendo vya ukatili vinavyoweza kuwapata wakiwa mazingira ya shuleni lakini pia katika mazingira ya makazi yao.


Ziara ya Mkurugenzi ilianza mara tu shule zilipofunguliwa Januari 8/2024 ambapo pamoja na kufuatilia  wanafunzi walioripoti  na wasioripoti pia amewataka watendaji wa kata na vijiji kuhakikisha wanafunzi wote ambao bado hawajaripoti shuleni kufikia Januari 20/2024 wawe wameripoti.


"Jukumu letu viongozi ni kufanya kazi kwa ufanisi, Serikali imejenga miundo mbinu mizuri sana katika shule sasa wanafunzi wasipokuwepo itafaa nini? Viongozi wa vijiji na kata wafuatilieni wale wote waliokaa na wanafunzi nyumbani hakikisheni wanaripoti kufikia Januari 20, Pia suala la chakula shuleni lazima lipewe umuhimu mkubwa na mikakati ya kuinua ufaulu  iwekwe na kuzingatiwa ili kufanikiwa haya yote hakikisheni nidhamu inapewa kipaombele kwa kila mmoja" Alisema Kihiyo.


Mpaka kufikia Januari 19/2024 tayari alikuwa ametembelea robo tatu ya shule zote zilizopo wilaya ya Chato imebainika kuwa ufuatiliaji huu wa shule kwa shule umezaa matunda kwa kiasi kikubwa kwani taarifa zimekuwa zikiwafikia wazazi waliokaa na wanafunzi nyumbani na kupelekea wimbi la kuripoti wanafunzi kuongezeka hivyo lengo la ziara  kutimia.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • JIMBO LA CHATO LAGAWANYWA RASMI

    May 12, 2025
  • CHATO TECHNICAL YAPONGEZWA

    May 09, 2025
  • WATAHINIWA 2234 WA KIDATO CHA SITA KUANZA MTIHANI MEI 5 WILAYANI CHATO

    May 04, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 01, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.