• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA CHATO YAANZA KUTOA HUDUMA KWA KISHINDO

Posted on: July 27th, 2022


Mkuu wa Wilaya ya Chato Martha Mkupasi ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya hiyo na maeneo jirani na mkoa wa Geita kwenda kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya Kanda iliyopo wilayani hapo kwani kwa sasa hospitali hiyoinavifaa vya kutosha na inatoa huduma za kibingwa kwa magonjwa yote.

Wito huo umetolewa leo kwenye ufunguzi wa juma la maadhimisho  mwaka mmoja wa utoaji huduma ya Hospitali hiyo ambayo ilianza kutoa huduma za rufaa tarehe 30 Julai 2021.

Mkuu wa Wilaya amesema kwa sasa hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato imepokea vifaa vingi hivyo ni vyema jamii ikaelewa kuwa hospitali hiyo ipo tayari kupokea wagonjwa wa aina yoyote kutoka maeneo ya karibu na mkoa wa Geita .

“Kwa sasa hospitali ina wataalamu wengi waliobobea, ina vifaa vingi na vizuri leo tumejionea wenyewe ndani ya hospitali hii, ni Imani yangu wagonjwa watatibiwa vizuri na kwa wakati” amesema Mkuu wa Wilaya ya Chato.

Mbunge wa jimbo la Chato Dkt. Medard Kalemani ameishukuru serikali ya awamu ya sita kuendelea kutoa fedha kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo ambapo amesema kukamilika kwa hospitali  hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato imesaidia wananchi wa Chato na mkoa wa Geita kwa ujumla kupatiwa matibabu kwa gharama nafuu na haraka kwani hapo awali walilazimika kwenda Mwanza kwa ajili ya matibabu.

“Mheshimiwa Rais atembee kifua mbele, fedha anazoleta tunaona zinafanya kazi nzuri, na sisi tunamhakikishia tutalinda miundombinu ya hospitali hii kwani matunda yake tunayaona” amesema Mhe. Dkt. Medard Kalemani

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Dkt. Oswald Lyapa amesema hospitali hiyo  imeweza kuhudumia wagonjwa 10,502 tangu ianze kutoa huduma tarehe 30 Julai 2021. Amesema wagonjwa wengi wanaopatiwa huduma wanatoka mikoa ya Geita, Kagera, Kigoma na Shinyanga.

Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato ilianza kujengwa mwaka 2017 na inakadiriwa kutoa huduma kwa wagonjwa 700 hadi 1000 kwa siku. Kwa sasa hospitali hiyo inatoa huduma za kibingwa za upasuaji, huduma za mama na mtoto, magonjwa ya ndani, huduma za utoaji dawa na vifaa tiba, huduma za uchunguzi wa afya na huduma za mionzi.

Hadi sasa ujenzi wa hospitali hiyo umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 25 ambapo kwa sasa serikali kupitia fedha za UVIKO 19 imetenga shilingi bilioni 6 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba ikiwa ni pamoja na CT Scan, MRI,X-Ray pamoja na vifaa vya wagonjwa mahututi na wagonjwa wa dharula.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.