• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

MILIONI 500 ZA MAPATO YA NDANI KUKAMILISHA KITUO CHA AFYA KATETE

Posted on: August 16th, 2022

Jumla ya wananchi 21,693 wa kata ya Bwongera wilayani Chato wanatarajia kunufaika na kituo kipya cha Afya cha kata hiyo kinachojengwa kwa mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo kinatarajiwa kugharimu shilingi milioni 500 pamoja na nguvu za wananchi.


Hayo yamebainishwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari ya Wilaya ya Chato ndugu Mandia Kihiyo wakati wa ziara ya kamati ya Fedha Uongozi na Mipango ya Halmashuri ikikagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri.


Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri kupitia mapato ya ndani ilitenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kujenga kituo cha hicho cha afya ikiwa ni sehemu ya fedha za asilimia 40 ya mapato ya ndani zinazotengwa kila mwaka kwa ajili ya miradi ya maendeleo.


"Hadi sasa tumekwishaleta hapa shilingi milioni 201 na lengo letu ni kukamilisha kituo hiki mwezi Septemba mwaka huu ambapo kwa mwaka huu tutajenga kituo kingine cha Afya Kata ya Ichwankima" alisema Mkurugenzi Mtendaji.


Mbunge wa Jimbo la Chato Mhe. Dkt. Medard Kalemani amepongeza baraza la Madiwani la Halmashauri kwa uamuzi wa kutenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kituo hicho ambapo amesema ujenzi wa kituo hicho ni maamuzi mazuri na ya kupongezwa ameomba kamati hiyo kuhakikisha kituo hicho kinakamilika kwa wakati ili kianze kutoa huduma.


"Nikupongeze Mkurugenzi na timu yako ya wataalamu,  mnafanya kazi nzuri sana, nimefanya kazi na wakurugenzi wengi lakini huyu anafanya kazi nzuri anastahili pongezi tusimkatishe tamaa" alisema Dkt. Kalemani


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Mhe. Christian Manunga ambaye pia ni diwani wa Kata ya Bwongera amesema kukamilika kwa kituo hicho kutanufaisha wakinamama wengi wa kata hiyo ambao wamekuwa wakipata  ugumu wakati wa kujifungua ambapo wamekuwa wakipata huduma katika zahanati ndogo iliyopo katika eneo hilo na wengine wamekuwa wakihudumiwa kwenye kituo cha Afya cha Muganza ambapo ni mbali kutoka eneo hilo.


Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Dkt. David Mndeba amesema kukamilika kwa kituo hicho kutasaidia wananchi wengi wakiwemo wa kata hiyo pamoja na Wilaya jirani ya Muleba ambao wamekuwa wakifika katika zahanati ya kijiji hicho.


Kituo cha Afya cha Katete kilianza kujengwa mwezi Desemba 2021 ambapo kuna jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la upasuaji na wodi ya wazazi ambapo jumla ya shilingi milioni 500 za mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na nguvu za wananchi zinatarajiwa kukamilisha kituo hicho mnano mwezi Septemba 2022.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.