• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

USIMAMIZI MAKINI WA MIRADI WABAKIZA CHENJI CHATO

Posted on: December 18th, 2024


Na Mwandishi wetu.

Mkuu wa wilaya ya Chato Mhe. Louis Bura akiwa ameambatana na kamati yake ya ulinzi na usalama pamoja na timu  ya wataalam ngazi ya wilaya wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya hiyo Dkt. Aristides Raphael, wametembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya wilaya hiyo.

Ziara hiyo imefanyika leo Disemba 18, 2024 ambapo miradi 11 imetembelewa na kukaguliwa, huku miradi mingi kati ya hiyo ikionekana kuridhisha na mingine kuibuka kidedea kwa ukamilishwaji wa haraka, viwango vya ubora pamoja na thamani ya fedha kuonekana huku chenji  ikibaki hususani mradi wa Bwalo la chakula Makurugusi Sekondari pamoja na Zahanati ya kijiji cha Butengorumasa.

Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa ni Ujenzi wa bwalo la chakula Makurugusi Sekondari (175,000,000/=), Shule mpya ya Igogo Sekondari - Buziku (114,400,000/=),  Nyumba ya watumishi 2 in 1, Mabweni 2 na vyoo matundu 12 Kabantange Sekondari (381,000,000/=), Jengo la X-rays Kituo cha afya Bwanga (58,468,176/=), Shule mpya ya Sekondari Mwendakulima (584,000,000/=), Shule Mpya ya kidato cha 5&6 Iparamasa (853,725,000/=), Ujenzi wa Daraja la Muranda - Imwelu (400,000,000/=), pamoja na ukaguzi wa utoaji huduma kituo cha afya Mapinduzi na kituo cha afya Iparamasa.


Mhe. Bura amewapongeza wasimamizi wa miradi hiyo kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya kwa umakini, kuhakikisha wanazingatia vigezo vya ubora wa majengo unaohitajika na Serikali huku akiwaasa wachache wenye changamoto katika ukamilishaji wa miradi kuhakikisha wanarekebisha tofauti zilizojitokeza na kuwataka wajifunze kwa waliofanikiwa.


"Ninawapongeza sana  wasimamizi kwa jinsi mnavyotekeleza miradi hii kwa ubora na thamani ya fedha inaonekana, lakini Shukrani nyingi zaidi ni kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wetu kwa kutuletea fedha nyingi sana za miradi ya maendeleo wilayani Chato, ni jukumu letu kuhakikisha tunasimamia vizuri ili kupata majengo yenye ubora na hatimaye nia ya Serikali yetu itimie watoto wetu waweze kukuta miundo mbinu imekamilika shule zitakapofunguliwa Januari 2025 lakini kwa upande wa afya tukamilishe ili huduma zianze kutolewa mapema kuwapunguzia umbali wananchi." Alisema Mhe. Bura.


Kwa upande wake diwani wa kata ya Butengorumasa Mhe. Makoye Daud Cosmas amekiri kufurahishwa na ukamilishwaji wa mradi wa zahanati ya kijiji hicho kwa wakati na kwa kubakiza chenji kwani  ilijengwa kwa nguvu za wananchi kwa Tsh. 19,521,000/=,  na kisha wakala wa misitu (TFS) kuwapatia kiasi cha Tsh 100,000,000/= ambayo walitumia 85,162,900/=kukamilisha zahanati hiyo na kusalia Tsh. 14,837,100/= fedha ambayo wataifanyia shughuli nyingine za maendeleo.


 " Ninaupongeza uongozi wote wa wilaya ya Chato kwa kuuweka mbele uzalendo katika kutekeleza miradi ya maendeleo, usimamizi madhubuti wa miradi kuanzia kwa Mhe. DC, Mkurugenzi, wataalam ngazi ya wilaya, Kata, pamoja na wasimamizi ngazi ya kijiji ndio chanzo cha mavuno bora ya miradi yetu hapa wilayani Chato, Serikali yetu ya awamu ya sita inafanya kazi kwa vitendo kila mmoja anapaswa kuiunga mkono kwa uaminifu na utii." Alisema. Cosmas

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • JIMBO LA CHATO LAGAWANYWA RASMI

    May 12, 2025
  • CHATO TECHNICAL YAPONGEZWA

    May 09, 2025
  • WATAHINIWA 2234 WA KIDATO CHA SITA KUANZA MTIHANI MEI 5 WILAYANI CHATO

    May 04, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 01, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.