• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

Posted on: April 16th, 2025


Wakazi wa Kijiji cha Kinsabe kata ya Iparamasa wilayani Chato mkoani Geita wameipongeza mamlaka ya usambazaji maji na Usafi wa Mazingira vijijini (Ruwasa) baada ya kuwanusuru na adha ya kutumia maji ya madimbwi kwa kishirikiana na fisi.

Aidha kijiji hicho hakijawahi kupata maji ya bomba tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika(Tanzania bara) na kwamba kitendawili hicho hatimaye kimeteguliwa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Pongezi hizo zimetolewa na Chausiku Bomba(65) mkazi wa kijiji hicho ambaye pamoja na mambo mengine amesema kabla ya Mradi huo walikuwa wakitumia maji machafu huku wakichangia na wanyama wa kufugwa na wale wa polini hali iliyokuwa ikiwasababishia kuugua magonjwa ya matumbo mara kwa mara.

Khadija Khamis, amesema upatikanaji wa maji hayo umesaidia baadhi ya wananchi kuvuta maji ya bomba kwenye makazi yao na kuondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kwenda kijiji jirani kutafuta huduma hiyo jambo lililo saidia kupatikana utulivu wa familia ukilinganisha na awali kabla ya kupatikana huduma ya maji ya bomba.

"Sasa hivi kwa kweli angalau tuna amani katika familia zetu,maana awali watoto wetu walikuwa wanatoka shule na kwenda kutafuta maji, lakini huko njiani wanakutana na vishawishi vya kila aina na wakati mwingine wanatishwa na fisi na kulazimika kurejea nyumbani bila maji" amesema Khadija.

Akielezea utekelezaji wa mradi huo mbele ya mkuu wa wilaya hiyo Meneja wa usambazaji wa maji na Usafi wa Mazingira vijijini(Ruwasa) wilaya ya Chato, Mhandisi Avitus Exavery, amesema mradi huo wa Kinsabe umekamilika kwa aslimia 98 na kwamba kaya 16 zimevuta maji majumbani huku zaidi ya wakazi 7,040 wanatarajia kunufaika kwa kutumia maji safi na salama.

Amesema mradi huo wa kisima kirefu chenye urefu wa mita 72 una uwezo wa kuzalisha lita za ujazo 12,000 kwa siku na kwamba umetekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 335.2 kwa lengo la kuondoa changamoto za upatikanaji wa maji kwa wananchi wa kijiji cha Kinsabe na vitongoji vya Beda,Kinsabe,Elimu, Nyangugunwa A na Nyangugunwa B.



Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.