• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

WWADAU WA MAENDELEO WAZIDI KUKIGH'ARISHA KITUO CHA AFYA MGANZA CHATO

Posted on: May 4th, 2023

Katika kuhakikisha Vituo vyote vya kutolea huduma za  Afya katika Halmashauri ya Chato vinatoa huduma bora, Shirika lisilol la Kiserikali (The Eleanor Foundation) limetoa msaada wa Magodoro 10 yenye thamani ya shilingi 1,200,000 ikiwa ni katika jitihada za kuhakikisha akina mama na watoto wanapata mazingira mazuri wakati wanapokwenda hospitalini hapo kupatiwa matibabu.


Akikabidhi msaada huo wa Magodoro Ndg. Sospeter Rwegoshora ambaye ni mjumbe wa bodi katika Shirika la Eleanor Foundation kwa niaba ya Shirika hilo ameiomba jamii kuonyesha mchango wake hasa katika maeneo wanayoomba kusaidiwa ili hata wao wanapokuwa wanapitia ni maeneo gani watoe msaada basi waanze na wale walioonyesha nia na utayari wa kupokea mradi au msaada ameongeza kwa kusema " unapoomba kusaidiwa anza wewe mwenyewe wengine wakikuona watakushika mkono pia kumbukeni mkono usiotoa na kupokea hakuna"


Aidha kwa nyakati nyingine Meneja Mradi shirika la Aleanor Foundation toka

Chato na Biharamulo Ndg. Godfrey Gahanga amewashukuru  viongozi wote wa Chama na Serikali kwa namna ambavyo wamekuwa bega kwa bega katika kuhakikisha Kituo cha Afya Mganza kinakuwa na mazingira mazuri ya kutolea huduma kwa wagonjwa.


Ndg. Gahanga ameongeza kwa kusema, katika kituo hiki cha Mganza huu sio msaada wetu wa kwanza mahala hapa tumekwisha saidia katika kuhakikisha kituo hiki kinapata maji safi na salama wakati wote na hiyo huduma teyari inafanya kazi pia huduma ya Solar kuhakikisha maeneo yote mhimu yanakuwa na umeme na mwanga wa uhakika mda wote mfano chumba cha kuhifadhia Damu, Maabara,  Chumba cha upasuaji na wodi ya wazazi japo nia yetu ni kuhakikisha kituo chote kinakuwa kimeunganisha na mfumo wa umeme wa Sola.


Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya Mganza amewashukuru sana Shirika la Eleanor Foundation kwa kusema "hakika sisi kama kituo hatuna cha kuwalipa ila kamwe hatutakuja kuwasahau kwani mmefanya mambo makubwa sana pengine bila ninyi tungechelewa sana kuwa na mazingira haya mazuri kwa ajili ya kutolea huduma kwa wagonjwa"


Akihitimisha hafla hiyo ya mapokezi ya msaada huo wa Magodoro Mganga Mkuu wa wilaya ya Chato Dr. Eugen amewashukuru wadau hao kwa kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na rafiki katika mazingira yao lakini pia amewaomba wasikomee Mganza tu bali wafike na vituo vingine kwani nako wanamahitaji mengi kama ambavyo Mganza imesaidiwa na sasa inag'ara kwelikweli.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSINGI WA MAENDELEO NI LAZIMA UTOKANE NA WANANCHI WENYEWE

    April 26, 2025
  • WADAU CHATO WATHIBITISHA MCHAKATO WA KUGAWANYA JIMBO UMEFATA TARATIBU ZOTE ZA VIKAO MBELE YA TUME HURU YA UCHAGUZI

    May 24, 2025
  • MILIONI 431.2 ZAWAGUSA WANANCHI SEKTA YA MAJI CHATO

    April 16, 2025
  • WANANCHI WA KINSABE WAISHUKURU RUWASA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI YA BOMBA

    April 16, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.