• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

SEKTA YA UVUVI

MAENDELEO YA UVUVI

Wilaya inaendesha Shughuli za uvuvi katika eneo la kilomita za mraba zipatazo 896 ndani ya ziwa Victoria. Aidha mkakati wa Wilaya kwa sasa ni kujielekeza katika uanzishaji wa mabwawa ya kufuga samaki kwenye maeneo ya kando kando ya ziwa, mito mikubwa na mabonde ya mpunga yenye uwezo wa kupata maji ya kutosha.

Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Wilayani Chato, unatumia Mfumo Shirikishi Jamii kupitia Vikundi vya Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Mwaloni (BMUs) ambapo kwa sasa Wilaya inazo BMU 24 na mialo rasmi 36, soko moja la Kimataifa Kasenda na Mwalo mmoja uliojengwa kijiji cha Kikumbaitale.

Masoko yanayochukua samaki hawa ni pamoja na viwanda vya kusindika samaki vya Mwanza, Musoma na Bukoba; masoko ya ndani ya Wilaya ni Kasenda, Bwanga, Buseresere, Buziku, Chato na Kasenga; masoko ya nje ya Wilaya ni kama Geita, Kahama, Runzewe, Bukoba, Biharamulo, Ngara, Mwanza, Kigoma, Dar es salaam, Dodoma, Shinyanga, Arusha na masoko ya nje ya nchi ni Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Zambia na Malawi.

 WAVUVI

Wilaya ina jumla ya wavuvi 3,336 kati yao, Wavuvi 3110, wanatumia vyombo vya uvuvi wengine wanatumia njia mbalimbali za asili.

UFUGAJI SAMAKI

Ufugaji wa samaki umeimarishwa zaidi kama njia mbadala ya kuongeza uzalishaji na kupunguza utegemezi wa samaki toka ziwani peke yake. Kwa sasa Wilaya inacho kituo 1 cha kuzalisha Vifaranga kilichopo kata ya Nyamirembe na Mabwawa 163 ya ufugaji wa samaki yaliyopo maeneo mbalimbali ndani ya wilaya.

 UVUVI HARAMU

Wilaya inaendelea na juhudi za kudhibiti uharibifu wa mazingira na uvuvi haramu kwa kutumia dhana shirikishi jamii kati ya Maafisa Uvuvi, Polisi, Vikundi vya Kusimamia Rasilimali ya Uvuvi Mwaloni (BMU) na Wenyeviti wa Vijiji.

Katika kutunza mazingira, vikundi vya BMU vimehamasishwa kufunga maeneo ya mazalia na makulio ya samaki kipindi cha mwezi Januari hadi Juni ya kila mwaka na Uvuvi haramu umeendelea kupigwa vita kupitia doria. Magari, mitumbwi na masoko ya samaki yameendelea kufanyiwa ukaguzi wa kushitukiza kwa lengo la kukamata samaki wachanga.

Kuanzia mwezi Januari hadi Desemba, 2017 Wilaya imefanikiwa kukamata nyavu haramu aina ya Timba 2,770 zenye thamani ya Tsh.221,600,000/=,  Kokoro 202 zenye thamani ya Tsh.202,000,000/= , Katuli 201 zenye thamani ya Tsh.402,000/=, nyavu ndogo za dagaa 99 zenye thamani ya Tsh.69,300,000/= , Tupatupa 45 zenye thamani ya Tsh.900,000/=, nyavu ndogo za makila 3,753 zenye thamani ya Tsh.18,765,000/= na mitumbwi 38 yenye thamani ya Tsh.11,400,000/= . Jumla ya nyavu 7,150 zenye thamani ya Tsh.525,207,000/=  zimeteketezwa kwa moto.Kama inavyoonekana kwenye jedwali hapa chini:-

Jedwali kuonesha takwimu za ukamataji wa nyavu haramu na thamani yake kuanzia mwezi Januari hadi Desemba, 2017;

Mwezi

Kokoro

 

Timba

 

Nyavu ndogo za makila

Katuli

Madema

Tupatupa

 

Nyavu za dagaa chani ya kiwango

Mitumbwi

JANUARI

4

70

112

-

-

-

8

3

FEBRUARI

15

114

360

14

-

3

-

6

MACHI

5

150

475

6

-

4

10

3

APRILI

8

106

506

3

-

2

2

7

MEI

20

44

204

2

-

5

1

-

JUNI

-

78

125

13

-

-

3

-

JULAI

-

644

151

-

-

-

5

5

AGOSTI

43

84

320

82

-

-

-

6

SEPTEMBA

28

74

116

32

-

-

6

-

OKTOBA

24

306

384

11

12

2

21

2

NOVEMBA

46

802

650

30

16

29

35

6

DESEMBA

19

298

350

8

14

-

8

-

Jumla

202

2770

3753

201

42

45

99

38

Thamani

202,000,000/=

221,600,000/=

18,765,000/=

402,000/=

840,000/=

900,000/=

69,300,000/=

11,400,000/=

 HATUA ZILIZOCHUKULIWA DHIDI YA WAVUVI HARAMU 

Kuanzia mwezi Januari hadi Desemba mwaka 2017 watuhumiwa 21 waliojihusisha na uvuvi haramu walifikishwa mahakamani ambapo jumla ya kesi 17 zilifunguliwa, katika  kesi 4 watuhumiwa wamefungwa mwaka mmoja na miezi sita,  kesi saba (7)watuhumiwa wamelipa faini na kesi sita (6) zinaendelea mahakamani.

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA UVUVI HARAMU

  • Watendaji wa Kata na Vijiji, Maafisa uvuvi wa Serikali kuu na wa Halmashauri,  Viongozi wa BMU pamoja na Wenyeviti wa Vijiji  wamesainishwa mikataba ya kuhakikisha maeneo yao hayapatikani na shughuli zozote za uvuvi haramu.
  • Kufanya doria za uvuvi mara kwa mara katika maeneo mbalimbali kwa kushirikiana na Wananchi.
  • Kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kukabiliana na uvuvi haramu.

MAFANIKIO YALIYOPATIKANA BAADA YA HATUA ZA KUPAMBANA NA UVUVI HARAMU

  • Samaki wachanga kupungua kwenye masoko
  • Kupatikana kwa samaki wakubwa wa kiwango kinachokubalika.
  • Wavuvi kuanza kutumia nyavu zinazokubalika kisheria.

Matangazo

  • MATOKEO YA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA CHATO WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI MAENEO YA BIASHARA STENDI MPYA KAHUMO January 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI January 03, 2022
  • View All

Habari Mpya

  • "NENDENI MKAWASAIDIE WAKULIMA WALIME KILIMO CHENYE TIJA WAACHANE NA KILIMO CHA MAZOEA" DC CHATO

    March 21, 2023
  • STENDI YA CHATO INAFANYA KAZI ACHENI UPOTOSHAJI

    March 16, 2023
  • SHAMLA SHAMLA ZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KATIKA HALMASHAURI YA CHATO ZAPAMBWA NA UTOAJI WA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 107 KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    March 08, 2023
  • "NENDENI MKATUMIE PIKIPIKI HIZI KWA KAZI ZA SERIKALI NASI VINGINEVYO" DED CHATO

    March 02, 2023
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.