• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Malalamiko |
    • Staff Mail |
Chato District Council
Chato District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofis ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chato

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Kilimo
      • Eduction
        • Primary
        • Secondary
      • Fedha
      • Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
      • Water
      • Works
      • Afya
      • Ardhi, na Maliasili
    • Vitengo
      • Procurement
      • ICT
      • Internal Audit
      • Legal
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uchimbaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Vivutio Vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Health Service
    • Education Service
    • Water Service
    • Agriculture Activities
    • Livestock Activities
    • Fisheries Activities
  • Councilors
    • Councilors List
    • Standing Committee
      • Finance, Planning & Administration
      • Education, Health & Water
      • Environment, Works & Economic
      • HIV/AIDS Control
      • Ethics
    • Schedule
      • Councilors Meting Schedule
      • Meet with Councilor
  • Miradi
    • Planned Projects
    • Miradi inayoendelea Kutekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Repoti
    • By Law
    • Fomu
    • Strategic Plan
    • Huduma ya Mkataba kwa Mteja
    • News Paper
  • Kituo vya Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Matukio
      • Habari

DED CHATO ATOA VYETI VYA PONGEZI KWA WAGANGA WAFAWIDHI KWA UTENDAJI KAZI HODARI

Posted on: July 31st, 2025

Leo Julai 31, 2025 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Chato, Mkoani Geita ametoa zawadi za vyeti vya pongezi kwa Waganga Wafawidhi wa Vituo vya Afya, Zahanati pamoja na Hospital ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wao katika ufanyaji kazi na utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Zawadi hizo zimetolewa kwa Vituo vya Afya vinne (4) ambavyo ni Butarama kipengere cha Mnyororo wa Ugavi (Supply Chain ELMIS Data), Iparamasa kipengere cha Usafi wa Mazingira, Bwanga kipengere cha Usimikaji na Matumizi ya GOT- HOMIS na Muganza kipengere cha Ukusanyaji wa Mapato yatokanayo na Huduma za Afya.

Kwa upande wa Zahanati ni vituo nane (8) tu vilivyopata zawadi hiyo ambavyo ni Nyamirembe na Ihanga kipengere cha Mnyororo wa Ugavi (Supply Chain EL-MIS Data), Bupandwampuli kipengere cha Usafi wa Mazingira na Buseresere kipengere cha Usimikaji na Matumizi ya GOT-HOMIS, Zahanati za Buseresere na Makurugusi kipengere cha Ukusanyaji wa Mapato yatokanayo na Huduma za Afya  nana mwisho ametoa zawadi Hospitali ya Wilaya kipengere cha Usafi wa Mazingira na Usimikaji na Matumizi ya mfumo wa GOT-HOMIS.

Akitoa zawadi hizo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndg. Mandia Kihiyo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri amewataka Waganga Wafawidhi, Wauguzi, Wahasibu na Makatibu wa Afya amewataka kila mmoja kwenda kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia maadili ya kazi na Utu wa Mtu, kusimamia Miradi ya Maendeleo kwa uadilifu na ubora unaotakiwa.

Aidha Ndg. Mandia amewataka Waganga na Wauguzi Wafawidhi kuhakukisha wanasimamia na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na watoto wachanga.

Akihitimisha Ndg. Mandia amewaasa Watumishi wote wa Umma kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa Amani na Utulivu huku akiwataka kutojihusisha na vitendo vinavyoweza kusababisha vurugu au kuondoa Amani ya Taifa letu.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya ya Chato Dkt. Daniel Mzee amemhakikishia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kuwa yeye pamoja na timu yake wamejipanga vizuri kuhakikisha maelekezo pamoja na maagizo yote aliyoyatoa yanakwenda kutekelezwa kwa ukamilifu na ubora.

Matangazo

  • MATOKEO YA UDEREVA CHATO DC September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI CHATO DC September 20, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO May 24, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI CHATO July 19, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • CMT YAFANYA ZIARA KUKAGUA UKAMILISHWAJI WA MIRADI YA MAJOSHO

    August 28, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAPEWA MAELEKEZO MAALUMU KAMPENI YA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU YA NG'OMBE

    August 28, 2025
  • WATUMISHI WAPYA IDARA YA KILIMO WAPEWA MAFUNDO NA MAZINGATIVU

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UCHUKUAJI FOMU ZA UBUNGE NA UDIWANI LINAENDELEA

    August 26, 2025
  • View All

Video

MHE. NDEJEMBI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA NA NIDHAMU NA KUTIMIZA WAJIBU KWA WELEDI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • HOTUBA YA BAJETI TAMISEMI 2019
  • Mwongozo wa Matumizi Bora na Salama wa Vifaa vya TEHAMA
  • MWONGOZO WA KUSIMAMIA NA KUENDESHA TOVUTI ZA SERIKALI
  • MWONGOZO WA OPRAS
  • TAARIFA KWA UMMA UFUNGUZI WA JENGO JIPYA JIPYA CRDB

Tovuti Linganifu

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais- TAMISEMI
  • eMrejesho - Malalamiko/taarifa yeyote kutoka kwa wananchi,Watumishi wa Umma/Wastaafu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Ofisi ya Rais- Utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    MKURUGENZI MTENDAJI

    Postal Address: 116 CHATO

    Telephone: +255282228007

    Mobile:

    Barua pepe: ded@chatodc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Malalamiko
    • map
    • Service

Copyright©2016 CDC . All rights reserved.